Monday, December 19, 2016
Sunday, December 18, 2016
BREAKING NEWS!!
Diwani wa Chadema Kata ya Boma Jimbo la Mafinga Mjini ndugu Kisoma amesimamishwa Udiwani na Tume ya Uchaguzi ya Taifa baada ya kuthibitika hajui kusoma na kuandika.
Friday, December 16, 2016
SERIKALI IMEJIPANGA KUHAKIKISHA SEKTA YA KILIMO INATOA MCHANGO KATIKA KUFIKIA NCHI YENYE UCHUMI WA VIWANDA
Na.Immaculate Makilika.
SERIKALI kupitia Wizara ya
Kilimo, Mifugo na Uvuvi imesema kuwa imeandaa mikakati mbalimbali ili
kuhakikisha Sekta ya Kilimo inatoa mchango zaidi katika kufikia nchi ya
uchumi wa kati.
Akizungumza Jijini Dar es Salaam
jana katika kipindi cha TUNATEKELEZA kinachoandaliwa na kituo cha televisheni cha TBC, aliyekuwa
Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo ambaye sasa ni Katibu Mkuu Wizara ya
Ulinzi Dkt. Florence Turuka alisema kuwa Serikali imeandaa mikakati hiyo
ili kuhakikisha kunakuwepo na uzalishaji wa mazao ya kilimo ili viwanda
viweze kupata malighafi, chakula cha kutosha pamoja na ajira kwa
wananchi.
“Serikali imeamua kuanzisha
viwanda vidogo vya kuchakata mazao kwa ajili ya soko, kushirikisha sekta
binafsi katika kuongeza thamani ya mazao, ili kuvutia wakekezaji katika
sekta ya kilimo nchini” alisema Dkt. Turuka.
Kwa mujibu wa Dkt. Turuka alisema
ili kuhakikisha huduma za ugani zinakua za kisasa Serikali
inadhamiria kutumia simu za mkononi zitakazorahisisha utoaji wa taarifa
kwa wataalamu wa kilimo, ikiwa ni pamoja na kusaidia wakulima kupata
huduma za kitaalamu kwa wakati.
Aidha Dkt. Turuka alisema
mikakati mingine inayotekelezwa na Serikali ni pamoja na kuongeza idadi
ya matrekta hadi kufikia 6,000 badala ya 400 yaliyokuwepo awali.
Aliongeza kuwa Serikali
imekusudia pia kujenga maghala karibu na maeneo yanayozalisha mazao ya
matunda na mbogamboga ili kuweza kuyahifadhi kwa muda kabla mazao hayo
hayajapekelekwa sokoni ili kupunguza uharibifu.
Naye Katibu Mkuu wa sasa wa
Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi, Mhandisi Mathew Mtigumwe alisema
Serikali itaboresha mfumo wa takwimu wa wataalamu wa kilimo pamoja na
kuwajengea uwezo ili kusaidia utekelezaji wa maendeleo ya kilimo katika
maeneo mbalimbali nchini.
Aidha, Serikali inawakaribisha
wawekezaji wa kilimo cha miwa ambapo imeandaa zaidi ya hekta 6000 kwa
ajili ya kilimo hicho nchini.
WATAYARISHAJI FILAMU WATAKIWA KUWA WABUNIFU.
Na. Genofeva Matemu.
Watayarishaji wa kazi za ubunifu ikiwemo filamu Tanzania wamehaswa kuwa wabunifu na kuacha kunakili kazi ambazo zilishafanywa na watu wengine kwani kwa kufanya hivyo hupelekea kudidimiza sekta ya Filamu na kuidhalilisha tasnia ya uigizaji nchini.
Watayarishaji wa kazi za ubunifu ikiwemo filamu Tanzania wamehaswa kuwa wabunifu na kuacha kunakili kazi ambazo zilishafanywa na watu wengine kwani kwa kufanya hivyo hupelekea kudidimiza sekta ya Filamu na kuidhalilisha tasnia ya uigizaji nchini.
Kauli
hiyo imetolewa na Katibu Tawala Mkoa wa Mara Bw. Ado Mapunda alipokua akifunga
warsha ya mafunzo ya kuwajengea uwezo wadau wa sekta ya filamu na michezo ya
kuigiza iliyofanyika kwa siku tatu na kufungwa leo Mkoani Mara.
“Tumieni
fursa hii ya kipekee kuchota maarifa ya kutosha yatakayowaongezea ujuzi katika
kazi zenu za filamu. Naamini baada ya warsha hii mtalenga kutoa kazi bora
zitakazokidhi mahitaji ya wadau wenu na pia zitakazoweza kushindana kwenye soko
la ndani na kimataifa” amesema Bw. Mapunda
Kwa upande wake Naibu
Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Bibi. Nuru Millao ameiomba
Ofisi ya Mkoa wa Mara na Wilaya zake kushirikiana na kuhimiza Sekta ya
Utamaduni kutengewa fedha kwa ajili ya maendeleo ya Filamu huku wakijumuishwa
katika fursa mbalimbali ikiwepo mikopo kupitia mfuko wa vijana na wanawake
ambapo itasaidia vijana na wanawake wengi
ambao wanajishughulisha na Tasnia ya filamu Kwa kuwa filamu inaweza kuchangia
ustawi wa uchumi kwa mtu mmoja mmoja na pia kuchangia pato la nchi kwa kiwango
kikubwa.
Naye katibu Mtendaji Bodi ya Filamu Bibi. Joyce
Fisoo amewaomba watayarishaji wa kazi za filamu kuwasilisha miswada yao kabla
ya kuandaa filamu zao ili bodi ya filamu ipate fursa ya kupitia miswada hiyo na
kuiboresha kabla ya filamu kuandaliwa jambo ambalo litasaidia kuondokana na
filamu zitakazokua zinazuiliwa kutokana na makosa madogo madogo yanayojitokeza
katika filamu zao.
Aidha
watayarishaji wa Mkoa wa Mara wametakiwa kutumia maarifa ya warsha hiyo
kutengeneza filamu zinazohamasisha uwajibikaji, umuhimu wa elimu kwa mtoto wa
kike, athari za ukeketaji, athari za uvuvi haramu kama baadhi ya maeneo ambayo
jamii ya Mkoa wa Mara inahitaji kuelimisha na kuondokana na dhana potofu.
Mafunzo
hayo yameshirikisha zaidi ya wadau wa sekta ya filamu na michezo ya kuigiza 200
kutoka Mkoa wa Mara, Halmashauri ya Manispaa ya Mosoma, Musoma Vijijini, Bunda
Mji, Tarime Mji, Halmashauri ya Wilaya ya Tarime, Lorya, Butihama na wadau
kutoka Mkoa jirani wa Simiyu.
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI.
WAZIRI
MKUU Kassim Majaliwa amemuagiza Mkuu wa Wilaya ya Ngorongoro, Bw. Rashid Taka
na Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo Bw. Raphael Siumbo kufanya uchunguzi na
kuwachukulia hatua watendaji wote watakaobainika kuhusika katika uuzwaji wa
kiwanja cha shule ya msingi Waso.
Ametoa
agizo hilo jana jioni (Alhamisi, Desemba 15, 2016) wakati akihutubia wananchi
katika mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye kata ya Waso Wilaya ya Ngorongoro
akiwa katika ziara ya kikazi mkoani Arusha.
Waziri
Mkuu alisema Serikali haiwezi kuvumilia kuona watendaji wachache wasiokuwa
waadilifu wanamega kiwanja cha shule na
kukiuza kwa maslahi yao, hivyo aliwataka viongozi hao kufuatilia na kumpa
taarifa ya hatua za kisheria walizochukua kwa wahusika.
“Mkuu
wa wilaya na Mkurugenzi hapa kuna malalamiko ya viwanja fuatilieni viwanja
hivyo vinavyolalamikiwa na wananchi ni viwanja gani je hiyo ya kwamba mmeuza
viwanja vya shule ameuziwa nani,” alisema.
Aidha,
Waziri Mkuu amemtaka Bw. Taka ahakikishe Mkuu wa Idara ya Ardhi, Maliasili na
Mzingira, Bw. Switbeth Byorushengo anatekeleza majukumu yake ipasavyo. Ametoa
agizo hilo baada ya wananchi kudai Ofisa huyo ameshindwa kufanya kazi na
kumuomba Waziri Mkuu aondoke naye.
Alisema
Bw. Byorushengo anatakiwa kuhakikisha halmashauri hiyo inapima viwanja vya
kutosha na kutoa hati kwa wananchi ili waweze kupata maeneo ya kujenga makazi
na shughuli zingine za kijamii.
Katika
hatua nyingine, Waziri Mkuu alimuagiza Mkurugenzi wa halmashauri hiyo Bw.
Byorushengo kuhakikisha halmashauri hiyo inaanza ujenzi wa hospitali ya wilaya
na ifikapo Aprili, 2017 awe amepewa taarifa za ulipofikia ujenzi huo.
Kwa
upande wake Mkurugenzi huyo alisema tayari wapo katika mchakato wa ujenzi wa
hospitali ya wilaya ambapo wametenga sh. milioni 800 za kuanzia.
Akizungumzia
kuhusu mgogoro wa ardhi kati ya vijiji vya Tarafa ya Loliondo na Hifadhi ya
Taifa ya Serengeti, Waziri Mkuu alitoa muda wa siku 30 kwa uongozi wa Shirika
la Hifadhi za Taifa Nchini (TANAPA) wawe wamekamilisha uhakiki wa mpaka huo.
Naye
Naibu Waziri wa Kilimo, Mifugo na Uvuvi ambaye ni Mbunge wa Ngorongoro
Mheshimiwa William Ole Nasha alimuomba Waziri Mkuu kuwasaidia kutatua mgogoro
huo wa ardhi kwa kuwa ni wa muda mrefu na unakwamisha shughuli za maendeleo.
Awali,
Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Bw. Mrisho Gambo alisema Wilaya ya Ngorongoro
inachangamoto nyingi ikiwemo ya ardhi na sasa kuna mgogoro kati ya Kampuni ya
Thomson Safari na wananchi ambao wanadai kuwa ardhi hiyo ilichukuliwa kinyemela
na mwekezaji huyo bila ya wao kushirikishwa.
Alisema
baada ya ziara ya Waziri Mkuu kumalizika mkoani hapa atarudi wilayani
Ngorongoro kwa ajili ya kutatua kero mbalimbali ikiwemo ya ardhi na matumizi
mabaya ya fedha zinazotolewa na wawekezaji ambazo matumizi yake hayajulikani.
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,
IJUMAA, DESEMBA 16, 2016.
MWILI WA BRIGEDIA JENERALI MHAIKI WAAGWA RASMI LEO.
JPM APONGEZWE URATIBU MAAFA KAGERA.
Na. Joseph Martin,
Nottingham
WATANZANIA bado
tuko katika masikitiko kufuatia maafa yaliyoletwa na tetemeko la ardhi mkoani
Kagera na baadhi ya maeneo ya Kanda ya Ziwa. Tetemeko hilo tunaambiwa ni la
kiwango cha skeli ya 5.7 ambayo ni kubwa.
Watu 17
wamefariki kutokana na tetemeko hilo, mamia wamejeruhiwa na maelfu ya nyumba
ama zimebomoka au zimeharibika kwa namna tofauti. Mimi binafsi nina ndugu zangu
ambao ni waathirika wa tukio hili na namshukuru Mungu kwa misaa waliyopata.
Nimefuatilia
sana yanayotokea kule Kagera na naendelea kufuatilia kwa sababu jamaa zetu wa
kule kwa kweli wanahitaji msaada wetu ingawa na wao pia wanapaswa kuchukua
hatua zao na za jamaa zao wa karibu katika kujinasua na janga lililowafika.
Maoni yangu leo
si ya kueleza tukio hilo wala kufafanua maafa yalivyowagusa ndugu, jamaa na
marafiki zetu, bali kimsingi, nimeandika kufikisha ujumbe kwa Mhe Rais wa Awamu
ya Tano, Dkt. John Pombe Magufuli. Nitaeleza kwa nini Dkt. Magufuli anapaswa
kupewa hongera zake katika hili.
Mosi, tufahamu
kuwa hili ni janga la asili na ni jambo
ambalo wanasayansi wanasema halitabiriki na hakuna mtu anaweza kujua lini
tetemeko la ardhi litatokea. Lakini hata tukijua, bado ni ngumu kuzuia athari
zake hasa kwa makazi na miundombinu.
Lakini tangu
kutokea kwa jambo hili, labda tofauti na ilivyopata kutokea katika majanga
mengine nchini kama vile mafuriko ya Kilosa na majanga mengine ya tetemeko au
mafuriko, kwa mara ya kwanza, na ikiwa haina uzoefu bado wa muda mrefu katika
uongozi, Serikali ya Magufuli imetuunganisha na imetutendea haki sana kwa
kiwango chake.
Mara tu baada ya
tukio, Waziri Mkuu alifika Kagera kuwajulia hali waathirika, kushiriki mazishi
ya umma ya waliofariki na kutoa maagizo kwa watendaji wake juu ya hatua za
haraka za kufanywa.
Mara tu baada ya
Waziri Mkuu kutoka Kagera, Rais Magufuli ambaye hata baadhi ya watendaji wake
waandamizi walishakuwa mjini Lusaka, Zambia alikokuwa aende kwa ajili ya
sherehe za kuapishwa Rais Lungu, naye aliahirisha safari hiyo.
Rais aliahirisha
safari na kubaki Dar es Salaam kuratibu kwa karibu maafa hayo na namna ya
kuwasaidia waathirika. Na mara moja tuliona athari za uwepo wake nchini ambapo
ilifanyika harambee Ikulu ambapo watanzania tukahamasishwa kuchangia.
Serikali ikachukua
hatua muhimu za mawasiliano na hamasa kwa wadau ikiwemo kutangaza akaunti ya
maafa na namba za simu za sisi kuchangia. Akaunti hizi, tofauti na miaka ya
nyuma zimesambazwa sana katika mitandao ya kijamii na hata nimeona matangazo
katika magazeti na katika televisheni. Mkuu wa Mkoa wa Kagera anatoa taarifa za
mara kwa mara pia.
Serikali pia
kupitia taasisi na wizara mbalimbali pia imeendesha matukio mengine ya
kuchangia waathirika, imeratibu nchi nyingine za kigeni na Balozi kupeleka
misaada Kagera na misaasa hiyo imeanza kuwafikia waathirika.
Nafahamu kuwa
Serikali haikuwa na wajibu wa moja kwa moja katika hili kwa kuwa haikusababisha,
lakini juhudi hizi ni za kupongezwa sana na za kukumbukwa sana. Mzee Magufuli
Mungu akutangulie.
Nnitumie fursa
hii pia kuwasihi watanzania wenzangu, katika kuwasaidia wenzetu, kama
tulivyoanza, kusiwe tena na siasa wala watu kutafuta upungufu na kukosoa. Kila
mmoja wetu “ajiongeze” wanasema vijana wa
mjini.
Hata kwa ndugu zangu
waathirika nao pia tujue sisi na jamaa zetu tuna jukumu la kwanza katika hili
na tujitume kujinasua katika janga hilo, Serikali inaweza kuleta kidogo cha
kuchangia au kutufuta machozi, au kurekebisha miundombinu ya umma lakini
tusibaki watu wa kusubiri tukidhani ndio tutafanyiwa kila kitu.
Hakuna
Serikalini duniani inayoweza kufanya kila kitu hasa yanapotokea majanga makubwa
hata ziwe na uwezo vipi. Niliwahi kufika Marekani kwenye eneo la janga la
Septemba 11 pale Manhttan, New York na kukuta hata baada ya miaka 10 eneo lile
halikuwa limeweza kurejea katika hali yake ya awali.
Kuna eneo kule
Japan baada ya maafa ya mafuriko nimepata kuvikuta vikiwa hadi leo haviko
katika sura yake ya awali. Naamini hata ndugu zangu wa Kagera wajue hili, yapo
mambo yanaweza kufanyika yakawa bora zaidi kwa jitihada zao na za Serikali,
lakini pia yapo yanayoweza kuchukua muda zaidi na au hata yasirejee katika
hatua kama za awali.
Nihitimishe, hongera
kwa JPM lakini pia Serikali na wadau wengine tuendeleze moyo huu huu na
ushirikiano huu huu katika matukio mengine mengi zaidi yawe ya maafa au ya
kawaida. Kama tulivyoungana katika suala la madawati na hili la maafa, naamini
tukiendelea kuungana pamoja, Tanzania itasonga mbele.
Nawashukuru
sana.
MAMBO 10 YALIYONIGUSA KATIKA MUSWADA WA HABARI.
Na. Joseph Sabinus, Nottingham University
JUZI niliandika makala
kuonesha kuwa kelele zinazoendelea kuhusu Muswada wa Sheria ya Huduma za Habari
ukizitazama kwa undani utakubaliana nami kuwa ni matokeo ya kada isiyojiamini.
Tasnia ya habari hapo
nchini haijiamini na hili linaweza kuelezwa ama na miaka mingi ya kuhangaika
kuwa na sheria yao huku zoezi hilo kila mara likikumbwa na sababu mbalimbali na
kuahirishwa au kwa namna wanavyojenga hoja zao.
Hata hivyo ukiziacha kelele
hizo na kuanza kuusoma muswada huu kwa kina na kwa kutafakari makosa mengi
yanayofanywa na vyombo vya habari popote duniani utakubaliana nami kuwa muswada
huu, kama walivyosema pia Tanganyika Law Society na Twaweza, una mambo mengi
mazuri na ni bora zaidi kuliko ile ya awali.
Nilidhani wanahabari
wangeshiriki vyema katika kuboresha yale maeneo yenye changamoto badala ya
kuwaachia watu wa tasnia nyingine. Ni bahati mbaya wadau hawa wamechagua kuwa
wanaharakati zaidi badala ya wanataaluma.
Binafsi baada ya kuusoma
muswada nimebaini masuala makubwa yafuatayo katika hili. Naomba tushirikiane.
1.
Sheria kutosajili mitandao
Awali nilipomsoma
Mbunge Zitto Kabwe nilistushwa kusikia kuwa sheria hii inalenga kubana hadi
mitandao ya kijamii. Hata hivyo sheria haisomwi kama gazeti.
Wakati Zitto alikuwa
akisoma tafsiri ya neno “media” na kuona limejumuisha mpaka mitandao ya
kijamii, ukweli ni kwamba ukiusoma muswada ule eneo ambalo sheria itahusika
nalo kwa maana ya uratibu ni sekta iitwayo “print media”
Kwa hiyo ni
kujidanganya kusema sheria hii itasajili mitandao ya kijamii na vitu
vinavyofanana na hivyo. Badala yake ukisoma kifungu cha 8(1) unauona ukweli
huu. Mitandao imekuwa kama chombo kingine cha habari lakini nadhani kuanza kuisajili sasa ni mapema mno.
2.
Habari ni
taaluma
Kwangu
mimi, sijui kwa wanahabari wenyewe, muswada huu unaleta kwa mara ya kwanza
mfumo madhubuti wa kuifanya sekta ya habari kuwa taaluma kamili na
itakayoheshimika na kutambuliwa zaidi.
Ukiutazama
mfumo unaopendekezwa wa Bodi ya Ithibati katika ibara ya 10 utaiona “spirit”
hii. Taaluma kuwa taaluma moja ya sifa ni hii. Lazima wanataaluma hiyo wawe na
Bodi inayowasajili kwa viwango vilivyowekwa. Hata hivyo sijapata sababu kwa
nini sifa hazijaanishwa kwa sasa.
3.
Bodi
kumilikiwa na wanahabari
Wakati nikiendelea
kuusoma muswada huu pia nilipatwa na wasiwasi kuhusu kuundwa kwa Bodi hiyo ya
Ithibati nikidhani ingejaa warasimu tunaowafahamu siku zote.
Hata hivyo kama kuna
jambo lingine la kuusifu muswada huu ni pamoja na muundo wa Bodi yake. Bodi
itakuwa na wajumbe 7 na kati ya hao wanne (4) watakuwa ni wanataaluma ya habari
akiwemo mwenyekiti wa Bodi.
Haya ni mapinduzi
makubwa katika uundaji wa Bodi za kitaaluma ambapo katika maeneo mengine
ingezingatiwa tu uwakilishi labda wa jinsi, umri au taasisi. Katika hili
tuwapongeze waliosanifu muundo wa Bodi hii.
4.
Bara Huru
lenye meno
Hapa nianze kwa
kusema muswada huu umechelewa sana na hakuna hoja wala haja ya kusubiri tena.
Wananchi wanahitaji kuhudumiwa na sekta bora zaidi ya habari na kila mmoja wetu
anajua umuhimu huu.
Ukisoma kifungu cha
23 na kuangalia majukumu yale ya Baraza Huru la Habari utakubaliana nami kuwa
tunahitaji Baraza hili Huru kuliko wakati wowote. Hilo Baraza linalotajwa
kuwepo ni NGO tu na Serikali yoyote duniani haiwezi kuendeshwa na NGO.
Baraza linaloundwa
humu nimeona litakuwa na uhuru na haki ya kutunga kanuni za maadili za
wanahabari na kuhakikisha wenyewe wanazielewa katika kuwasimamia kwenye kazi
zao. Hii ni muhimu sana.
Ukienda Mahakamani
inachukua miaka. Ukienda MCT ya sasa hata wakitoa uamuzi chombo cha habari
kinakuwa na uhuru wa kuukataa au kuukubali uamuzi huo. Baraza hili kwa kuwa
limeanzishwa kisheria na lina nguvu za kisheria litakuwa na uwezo wa kusimamia
hata utekelezaji wa hukumu zake.
5.
Wanahabari
kutunga kanuni zao
Katika
hili niseme tu kwamba kama kuna jambo wanahabari wamekuwa wakilikosa kwa muda sasa
ni kwanza kuwa na chombo kimoja kinachowaunganisha bila kuwabagua zaidi ya wao
tu kuwa wanahabari.
Katika
Baraza linaloanzishwa nimeona vifungu kuwa litakuwa na kazi nyingine muhimu na
ya kipekee (exclussive rights) ya kuandaa kanuni za maadili (media code of
ethics). Hii ni muhimu kwa sababu badala ya kutungiwa na watu wengine ni
wanahabari wenyewe watakaozitunga kwa sababu pia wanafahamu vyema kazi yao.
6.
Kamati ya
malalamiko
Kumekuwa
na fikra miongoni mwa watu kuwa kuipata haki mahakamani ni gharama kubwa sana
na inayochukua muda mrefu. Katikati ya keleleza za baadhi ya watu kuwa sheria
hii haina jema, ni muhimu kuona umuhimu wa kifungu hiki.
Kwa
kuanzishwa Kamati ya Malalamiko chini ya Baraza Huru la Habari, sasa wananchi
watapata pa kulalamikia na tena penye meno. Lazima tukubali kuwa ama kwa ajenda
fulani au makosa ya kibinadamu, vyombo vya habari nchini vinawakosea sana watu
binafsi au taasisi.
Naamini
ni vyema kuwapa wahusika mahala pa kulalamika kwa sababu kwenda Mahakamani ni
suala ambalo kila mmoja, kwa sababu tulizokwishaeleza, asingependa kulichagua.
Kamati hii basi ikiundwa itoe uamuzi kwa haraka na iwe madhubuti.
7.
Bima ya
Afya
Mwezi
Novemba mwaka jana nilirejea nchini kwa mapumziko ya mwisho wa mwaka. Katika
pita pita zangu jijini Dar es Salaam nilikutana na matukio mawili ya wanahabari
kuchangiwa na wenzao.
Nilipofuatilia
suala hili nikaambiwa kuwa wanahabari hao hawakuwa na bima na walipopatwa na
maradhi ya muda mrefu ikawalazimu kuishi na kupata tiba kupitia michango ya
kujitolea ya wanataaluma wenzao.
Wapo pia waandishi
ambao hadi sasa wako hai lakini wanaishi kwa kutegemea misaada ya ndugu na
jamaa kwa ajili ya kupata huduma za afya. Nauona muswada huu unakuja kuwakomboa
wanahabari. Ni muswada unaokuja kuhakikisha kuwa si tu wanataaluma hii
wanafanya kazi zao kwa ufasaha lakini pia waweze kupata haki yao ya matibabu na
kuwekewa hifadhi ya jamii.
Iliniuma
na leo tunapoona katika kifungu cha 58 cha muswada huu kuna ulazima kwa
wamiliki wa vyombo vya habari kuwakatia bima watu wao, inashangaza kuona wapo
wanahabari ambao wanadai muswada huu haufai na kutaka urejeshwe nyuma.
8.
Haki za
watu
Ukisoma
Tamko la Haki za Binadamu la 1948 utaona msingi wa haki kuwa umebebwa katika
dhana ya haki ya mtu mmoja hukoma pale utekelezaji wa haki hiyo unapoingilia
uhuru au haki ya mtu mwingine.
Nimeviona
vifungu kadhaa vya muswada huu vikiwa na mlengo huu wa kuhakikisha wakati, kwa
mfano, haki ya wanahabari kukusanya na kusambaza habari ikiwa ni muhimu, pia
ziko haki za watu wengine zinazopaswa kulindwa na wanahabari.
Kifungu
cha 32 katika hili kwa mfano kinaainisha au kukataza waandishi kuchapisha kashifa
na kuwashushia watu wengine hadhi zao bila sababu (wawe hai au wamekufa). Hii
ni muhimu sana.
9.
Usalama wa Nchi
Nikikumbuka jinsi
vyombo vya habari vilivyochangia katika machafuko katika nchi mbalimbali
duniani hasa Rwanda (1994) na Kenya (2007) nashawishika kuchekelea ninapousoma
muswada huu.
Ukiacha vifungu
vinavyoainisha uchochezi, nimeguswa zaidi na kifungu cha 55 cha Sheria
kinapompa mamlaka Waziri akijiridhisha kuwa kuna suala linalokwenda kukiuka
usalama wa nchi basi achukue hatua haraka.
Wanaharakati hupinga
vifungu kama hivi kwa hoja za juu juu tu za kutokuwaamini viongozi wanaoweza
kupewa madaraka hayo, lakini uhalisi kwamba mambo haya yameshatokea na kwamba
zipo nchi zimeshawahi kuingia katika umwagaji wa damu kwa vyombo vya habari
kuachwa huru watakavyo, mtu hawezi kubeza kuwekwa kwa vifungu kama hivi.
Lipo pia kosa
la uchochezi ambalo wengi, bila kulitafakari, wanapiga kelele zilizokosa
tafakuri. Unawezaje kuwaacha watu watumie vyombo vya habari kuchochea vurugu,
kuhamaisha uasi na machafuko katika nchi? Kwangu mimi makosa kama haya ni muhimu
kwa usalama wa nchi na ni juu ya kila mmoja kutekeleza sheria.
10. Kufutwa
sheria ya Magazeti
Mimi nikiwa hapo
nyumbani kwa miaka mingi nimekisikia kilio cha wadau dhidi ya Sheria ya
Magazeti, 1976. Sheria hii tumekua nayo, tumeishi nayo na tulianza kuzeeka nayo
lakini kila mwanataaluma akijua haikuwa sheria nzuri.
Kwamba leo inafutwa
ni faraja kwa tasnia na nilidhani wenzetu wengine badala ya kulaani jambo hili wangeungana
nasi kulishangilia. Kwangu, kama kuna jambo jingine kubwa kwa wanatasnia
kulishangilia ni kufutwa kwa sheria hii ambayo wengine walifikia hatua ya
kuiita “ya kikatili.”
Wakati nikiamini
wabunge watakuwa wamefanyiakazi changamoto nyingine na kuuboresha muswada
katika maeneo machache kama vile kukamatwa mitambo kabla ya uamuzi wa mahakama
na kuainishwa viwango vya taaluma, niwaase wanahabri nchi kuwa katika ulimwengu
wa utatuzi wa migogoro; mazungumzo ni muhimu.
Ni bahati mbaya
kwamba katika hili walichagua kutozungumza na Kamati ya Bunge na wakasusia na
hatimaye muswada huu ukipita utawahusu hata kama wao hawakushiriki kuutunga.
*Mwandishi wa makala haya
amejitambulisha kuwa ni mwanafunzi wa shahada ya uzamivu (PhD) kwenye Chuo
Kikuu cha Nottingham, Uingereza.
BUNGE LAIGOMEA SERIKALI KUSAINI EPA.
Na Mwandishi Wetu–Dodoma
Mkutano
wa Tano wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania umeizuia Serikali
kusaini Mkataba wa Makubaliano ya Ushirikiano wa Kiuchumi Kati ya
Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) na Jumuiya ya Ulaya (EU) – (EPA) kwa
kuwa hauna manufaa kwa nchi ya Tanzania.
Uuamuzi huo
umetolewa leo mjini Dodoma na wabunge wa Bunge hilo baada ya kuujadili
mkataba huo kwa kina kwa kutoa maoni yao ambapo wengi wameunga mkono
kutosainiwa kwa mkataba huo.
Baadhi
ya wabunge waliopata nafasi ya kutoa maoni yao katika mjadala huo ni
pamoja na mbunge wa Mtwara Vijijini, Mhe. Hawa Ghasia ambaye amemshauri
Mhe. Rais Dkt .John Pombe Magufuli kutosaini mkataba huo kwa kuwa una
hasara nyingi kwa taifa kuliko faida.
”Kwa
kuzingatia mkataba umeruhusu uingizaji na utoaji wa bidhaa huru na
ukizingatia hakuna nchi hata moja ya Ulaya ambayo Tanzania inapeleka
bidhaa zake hivyo mkataba huu hauna maslahi kwa watanzania”, alisema
Mhe. Ghasia.
Aliongeza
kuwa Tanzania sio nchi ya kwanza kutosaini mkataba huo kwani kuna nchi
kama Angola, Nigeria, na Gambia hazijasaini,ameongeza kuwa kama Tanzania
itakubaliana na mkataba huo utaua viwanda pamoja na biashara za
Tanzania.
Kwa
upande wake Mbunge wa Nzega Mjini (CCM), Mhe.Hussein Bashe alisema kuwa
tatizo lililopo katika mkataba huo ni kutoitambua nchi kama nchi na
badala yake kuangalia nchi zote kwa pamoja hivyo amewashauri wabunge
kuhoji kuanzia kwenye kiini cha tatizo.
“Kwa
kuwa kifungu cha 143 cha mkataba huo kinaruhusu kupeleka marekebisho,
naishauri Serikali yetu ipeleke marekebisho ya kupendekeza kila nchi
iingie mkataba kivyake kulingana na maslahi ya nchi yake”, alisema
Bashe.
Aidha,
Mbunge wa Mwibara Mhe.Kangi Lugola (CCM) alimpongeza Mhe. Rais Magufuli
kwa kusita kusaini mkataba huo kwani ni miongoni mwa mikataba mibovu
kati ya mikataba iliyowahi kuletwa nchini kutoka katika nchi za Ulaya.
“Kama
tukikubali kusaini mkataba huu nchi hii itakuwa dampo la bidhaa
mbalimbali za ajabu kutoka nje na hivyo kupelekea kushindwa kutimiza
dhamira ya nchi ya kuimarisha viwanda vyetu”, alisema Mhe. Lugola.
Naye,
Mbunge wa Mchinga Mhe. Hamidu Bobali alisema kuwa mkataba huo haufai
kwa maslahi mapana ya taifa hili kwani unataka kuondoa ushuru kwa bidhaa
zinazoingia nchini wakati nchi ya Tanzania inaingiza bidhaa nyingi
kutoka nje kuliko kupeleka bidhaa nje ya nchi.
“Kama
tukikubali tukaondoa ushuru wa kuingiza bidhaa kutoka nje basi
tutapoteza mapato mengi yanayotokana na kuwepo kwa bandari pia
tunatakiwa tujiulize kama mkataba umeruhusu uingizaji na utoaji wa
bidhaa huru je nchi yetu ina bidhaa zinazokidhi vigezo vya kuingia
katika nchi za Ulaya?” , alihoji Mhe. Bobali.
Mhe.
Bobali ametoa rai kwa Serikali kuileta Bungeni mikataba mikubwa kama ya
gesi na madini kwa ajili ya kujadiliwa kwa kina ili kuepuka kusaini
mikataba isiyo na tija kwa Taifa.
Baada
ya majadiliano hayo hatimaye Bunge limepitisha Azimio la
kuitaka Serikali kutosaini mkataba huo kwa sababu umeonekana kuwa na
mapungufu yanayohitaji marekebisho ambayo yataleta maslahi kwa Taifa.
MAGUFULI GETS "STOP ORDER" FROM NATIONAL ASSEMBLY ON EPA.
By. Staff Reporter, Dar es Salaam
ATTEMPTS by the fifth phase government
of Tanzania under President John Pombe Magufuli to reconsider whether or not to
sign the Economic Partnership Agreement (EPA) have been thwarted by the country’s
National Assembly.
During the last East African
Community Heads of States Summit in Dar es Salaam, the partner states allowed
more time for consultations. Specifically, Tanzania, needed more time to
reconsider the various options on the economic partnership.
But the resolution made by the
country’s National Assembly in session in Dodoma to stop the government from
signing the EPA agreement in its current form, means President Magufuli’s
options are minimized.
Constitutionally, a resolution of the
National Assembly as an important pillar of the government is a binding
advisory, says a law Professor based in Dar es Salaam.
Reports from Dodoma reveal that most
Members of the Assembly contributed against any move to sign the agreement.
Most of them citing the lack of protection of local industries if the current
EPA document is signed, said the Agreement has to undertake comprehensive
amendments.
In July, 2016 the Kenyan Daily Nation
newspaper quoted some European MPs as backing efforts not to sign the deal to
allow more time for consultations.
Subscribe to:
Posts (Atom)