Sunday, December 18, 2016

BREAKING NEWS!!

Diwani wa Chadema Kata ya Boma Jimbo la Mafinga Mjini ndugu Kisoma amesimamishwa  Udiwani na Tume ya Uchaguzi ya Taifa baada ya kuthibitika hajui kusoma na kuandika.

Friday, December 16, 2016

SERIKALI IMEJIPANGA KUHAKIKISHA SEKTA YA KILIMO INATOA MCHANGO KATIKA KUFIKIA NCHI YENYE UCHUMI WA VIWANDA

Na.Immaculate Makilika.

SERIKALI kupitia Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi imesema kuwa imeandaa mikakati mbalimbali  ili kuhakikisha Sekta ya Kilimo  inatoa mchango zaidi katika kufikia nchi ya uchumi wa kati.

Akizungumza Jijini Dar es Salaam jana katika kipindi cha TUNATEKELEZA kinachoandaliwa na kituo cha televisheni cha TBC, aliyekuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo ambaye sasa ni Katibu Mkuu  Wizara ya Ulinzi Dkt. Florence Turuka alisema kuwa Serikali imeandaa mikakati hiyo ili kuhakikisha kunakuwepo na uzalishaji wa mazao ya kilimo ili viwanda viweze kupata malighafi, chakula cha kutosha pamoja na ajira kwa wananchi.

“Serikali imeamua kuanzisha viwanda vidogo vya kuchakata mazao kwa ajili ya soko, kushirikisha sekta binafsi katika kuongeza thamani ya mazao, ili kuvutia wakekezaji katika sekta ya kilimo  nchini” alisema Dkt. Turuka.

Kwa mujibu wa Dkt. Turuka alisema ili kuhakikisha huduma za ugani zinakua za kisasa   Serikali inadhamiria kutumia simu za mkononi zitakazorahisisha utoaji wa  taarifa kwa wataalamu wa kilimo, ikiwa ni pamoja na kusaidia wakulima kupata huduma za kitaalamu kwa wakati.

Aidha Dkt. Turuka alisema mikakati mingine inayotekelezwa na  Serikali ni pamoja na kuongeza idadi ya  matrekta hadi kufikia 6,000 badala ya 400 yaliyokuwepo awali.
Aliongeza kuwa Serikali imekusudia pia kujenga maghala karibu na maeneo yanayozalisha mazao ya matunda na mbogamboga ili kuweza kuyahifadhi kwa muda kabla mazao hayo hayajapekelekwa sokoni ili kupunguza uharibifu.

Naye Katibu Mkuu wa sasa wa Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi, Mhandisi Mathew Mtigumwe alisema Serikali itaboresha mfumo wa takwimu wa wataalamu wa kilimo pamoja na kuwajengea uwezo ili kusaidia utekelezaji wa maendeleo ya kilimo katika maeneo mbalimbali nchini.

Aidha, Serikali inawakaribisha wawekezaji wa kilimo cha miwa ambapo imeandaa zaidi ya hekta 6000 kwa ajili ya kilimo hicho nchini.

WATAYARISHAJI FILAMU WATAKIWA KUWA WABUNIFU.

Na. Genofeva Matemu.

Watayarishaji wa kazi za ubunifu ikiwemo filamu Tanzania wamehaswa kuwa wabunifu na kuacha kunakili kazi ambazo zilishafanywa na watu wengine kwani kwa kufanya hivyo hupelekea kudidimiza sekta ya Filamu na kuidhalilisha tasnia ya uigizaji nchini.

Kauli hiyo imetolewa na Katibu Tawala Mkoa wa Mara Bw. Ado Mapunda alipokua akifunga warsha ya mafunzo ya kuwajengea uwezo wadau wa sekta ya filamu na michezo ya kuigiza iliyofanyika kwa siku tatu na kufungwa leo Mkoani Mara.

“Tumieni fursa hii ya kipekee kuchota maarifa ya kutosha yatakayowaongezea ujuzi katika kazi zenu za filamu. Naamini baada ya warsha hii mtalenga kutoa kazi bora zitakazokidhi mahitaji ya wadau wenu na pia zitakazoweza kushindana kwenye soko la ndani na kimataifa” amesema Bw. Mapunda

Kwa upande wake Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Bibi. Nuru Millao ameiomba Ofisi ya Mkoa wa Mara na Wilaya zake kushirikiana na kuhimiza Sekta ya Utamaduni kutengewa fedha kwa ajili ya maendeleo ya Filamu huku wakijumuishwa katika fursa mbalimbali ikiwepo mikopo kupitia mfuko wa vijana na wanawake ambapo itasaidia vijana na wanawake  wengi ambao wanajishughulisha na Tasnia ya filamu Kwa kuwa filamu inaweza kuchangia ustawi wa uchumi kwa mtu mmoja mmoja na pia kuchangia pato la nchi kwa kiwango kikubwa.

Naye katibu Mtendaji Bodi ya Filamu Bibi. Joyce Fisoo amewaomba watayarishaji wa kazi za filamu kuwasilisha miswada yao kabla ya kuandaa filamu zao ili bodi ya filamu ipate fursa ya kupitia miswada hiyo na kuiboresha kabla ya filamu kuandaliwa jambo ambalo litasaidia kuondokana na filamu zitakazokua zinazuiliwa kutokana na makosa madogo madogo yanayojitokeza katika filamu zao.

Aidha watayarishaji wa Mkoa wa Mara wametakiwa kutumia maarifa ya warsha hiyo kutengeneza filamu zinazohamasisha uwajibikaji, umuhimu wa elimu kwa mtoto wa kike, athari za ukeketaji, athari za uvuvi haramu kama baadhi ya maeneo ambayo jamii ya Mkoa wa Mara inahitaji kuelimisha na kuondokana na dhana potofu.

Mafunzo hayo yameshirikisha zaidi ya wadau wa sekta ya filamu na michezo ya kuigiza 200 kutoka Mkoa wa Mara, Halmashauri ya Manispaa ya Mosoma, Musoma Vijijini, Bunda Mji, Tarime Mji, Halmashauri ya Wilaya ya Tarime, Lorya, Butihama na wadau kutoka Mkoa jirani wa Simiyu.

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI.

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amemuagiza Mkuu wa Wilaya ya Ngorongoro, Bw. Rashid Taka na Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo Bw. Raphael Siumbo kufanya uchunguzi na kuwachukulia hatua watendaji wote watakaobainika kuhusika katika uuzwaji wa kiwanja cha shule ya msingi Waso.
Ametoa agizo hilo jana jioni (Alhamisi, Desemba 15, 2016) wakati akihutubia wananchi katika mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye kata ya Waso Wilaya ya Ngorongoro akiwa katika ziara ya kikazi mkoani Arusha.
Waziri Mkuu alisema Serikali haiwezi kuvumilia kuona watendaji wachache wasiokuwa waadilifu  wanamega kiwanja cha shule na kukiuza kwa maslahi yao, hivyo aliwataka viongozi hao kufuatilia na kumpa taarifa ya hatua za kisheria walizochukua kwa wahusika.
“Mkuu wa wilaya na Mkurugenzi hapa kuna malalamiko ya viwanja fuatilieni viwanja hivyo vinavyolalamikiwa na wananchi ni viwanja gani je hiyo ya kwamba mmeuza viwanja vya shule ameuziwa nani,” alisema.
Aidha, Waziri Mkuu amemtaka Bw. Taka ahakikishe Mkuu wa Idara ya Ardhi, Maliasili na Mzingira, Bw. Switbeth Byorushengo anatekeleza majukumu yake ipasavyo. Ametoa agizo hilo baada ya wananchi kudai Ofisa huyo ameshindwa kufanya kazi na kumuomba Waziri Mkuu aondoke naye.
Alisema Bw. Byorushengo anatakiwa kuhakikisha halmashauri hiyo inapima viwanja vya kutosha na kutoa hati kwa wananchi ili waweze kupata maeneo ya kujenga makazi na shughuli zingine za kijamii.
Katika hatua nyingine, Waziri Mkuu alimuagiza Mkurugenzi wa halmashauri hiyo Bw. Byorushengo kuhakikisha halmashauri hiyo inaanza ujenzi wa hospitali ya wilaya na ifikapo Aprili, 2017 awe amepewa taarifa za ulipofikia ujenzi huo.
Kwa upande wake Mkurugenzi huyo alisema tayari wapo katika mchakato wa ujenzi wa hospitali ya wilaya ambapo wametenga sh. milioni 800 za kuanzia.
Akizungumzia kuhusu mgogoro wa ardhi kati ya vijiji vya Tarafa ya Loliondo na Hifadhi ya Taifa ya Serengeti, Waziri Mkuu alitoa muda wa siku 30 kwa uongozi wa Shirika la Hifadhi za Taifa Nchini (TANAPA) wawe wamekamilisha uhakiki wa mpaka huo.
Naye Naibu Waziri wa Kilimo, Mifugo na Uvuvi ambaye ni Mbunge wa Ngorongoro Mheshimiwa William Ole Nasha alimuomba Waziri Mkuu kuwasaidia kutatua mgogoro huo wa ardhi kwa kuwa ni wa muda mrefu na unakwamisha shughuli za maendeleo.
Awali, Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Bw. Mrisho Gambo alisema Wilaya ya Ngorongoro inachangamoto nyingi ikiwemo ya ardhi na sasa kuna mgogoro kati ya Kampuni ya Thomson Safari na wananchi ambao wanadai kuwa ardhi hiyo ilichukuliwa kinyemela na mwekezaji huyo bila ya wao kushirikishwa.
Alisema baada ya ziara ya Waziri Mkuu kumalizika mkoani hapa atarudi wilayani Ngorongoro kwa ajili ya kutatua kero mbalimbali ikiwemo ya ardhi na matumizi mabaya ya fedha zinazotolewa na wawekezaji ambazo matumizi yake hayajulikani.
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,
IJUMAA, DESEMBA 16, 2016.

MWILI WA BRIGEDIA JENERALI MHAIKI WAAGWA RASMI LEO.

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (katikati) akifuatana na Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa Dkt.Hussein Ali Mwinyi  (kushoto) na Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Tanzania Jenerali Davis Mwamunyange (kulia)wakati Rais alipofika leo katika Hospitali ya Jeshi la Wananchi JWTZ Lugalo Dar es Salaam kwa ajili ya kuuaga mwili wa Marehemu Brigedia Jenerali Cyril Ivor Mhaiki aliyekua Kamanda wa Brigedi ya Nyuki Zanzibar,aliyefariki juzi hospitalini hapo baada ya kuugua kwa muda mfupi.

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akitia saini kitabu cha kumbukumbu ya Marehemu Brigedia Jenerali Cyril Ivor Mhaiki, aliyekua Kamanda wa Brigedi ya Nyuki Zanzibar,ambae alifariki juzi katika  hospitali  ya Jeshi la Wananchi JWTZ Lugalo JIjini Dar es Salaam,baada ya kuugua kwa muda mfupi na kuagwa leo

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (katikati) Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa Dkt.Hussein Ali Mwinyi  (kushoto) na Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Tanzania Jenerali Davis Mwamunyange (kulia) wakiwa katika Kambi ya Jeshi la Wananchi Lugalo Dar es Salaam leo   kuuaga mwili wa Marehemu Brigedia Jenerali Cyril Ivor Mhaiki aliyekua Kamanda wa Brigedi ya Nyuki Zanzibar,aliyefariki juzi katika hospitali ya Jeshi la Wananchi JWTZ Lugalo, baada ya kuugua kwa muda mfupi.

Baadhi ya Maafisa wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania JWTZ waliofika leo katika hafla ya kuuaga Mwili wa Marehemu Brigedia Jenerali Cyril Ivor Mhaiki aliyekua Kamanda wa Brigedi ya Nyuki Zanzibar,aliyefariki juzi katika hospitali ya Jeshi la Wananchi JWTZ Lugalo, baada ya kuugua kwa muda mfupi,ambapo utaagwa leo katika Hospitali Lugalo Dar es Salaam.

Wananchi mbali mbali na jamaa waliofika leo   kuuagawa  Mwili wa Marehemu Brigedia Jenerali Cyril Ivor Mhaiki aliyekua Kamanda wa Brigedi ya Nyuki Zanzibar,aliyefariki juzi katika hospitali ya Jeshi la Wananchi JWTZ Lugalo Dar es Salaam, baada ya kuugua kwa muda mfupi.

Jeneeza lenye Mwili wa Marehemu Brigedia Jenerali Cyril Ivor Mhaiki  aliyekua Kamanda wa Brigedi ya Nyuki Zanzibar,aliyefariki juzi katika hospitali  ya Jeshi la Wananchi JWTZ Lugalo   Dar es Salaam,ukibebwa  na askari kupelekwa sehemu maalum ambapo utaagwa rasmi leo kabla kupelekwa kijijini kwao kwa mazishi.

Mawaziri wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar na Viongozi pamoja na Wazee wa Chama leo walijumuika na Maaskari wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania katika kuuaga Mwili wa Marehemu Brigedia Jenerali Cyril Ivor Mhaiki aliyekua Kamanda wa Brigedi ya Nyuki Zanzibar,aliyefariki juzi katika hospitali ya Jeshi la Wananchi JWTZ Lugalo Dar es Salaam, baada ya kuugua kwa muda mfupi.

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein alipokuwa akitoa heshima ya mwisho leo kwa mwili wa Marehemu Brigedia Jenerali Cyril Ivor Mhaiki aliyekua Kamanda wa Brigedi ya Nyuki Zanzibar,aliyefariki juzi katika hospitali ya Jeshi la Wananchi JWTZ Lugalo Dar es Salaam, baada ya kuugua kwa muda mfupi.


JPM APONGEZWE URATIBU MAAFA KAGERA.

Na. Joseph Martin, Nottingham  
WATANZANIA bado tuko katika masikitiko kufuatia maafa yaliyoletwa na tetemeko la ardhi mkoani Kagera na baadhi ya maeneo ya Kanda ya Ziwa. Tetemeko hilo tunaambiwa ni la kiwango cha skeli ya 5.7 ambayo ni kubwa.

Watu 17 wamefariki kutokana na tetemeko hilo, mamia wamejeruhiwa na maelfu ya nyumba ama zimebomoka au zimeharibika kwa namna tofauti. Mimi binafsi nina ndugu zangu ambao ni waathirika wa tukio hili na namshukuru Mungu kwa misaa waliyopata.

Nimefuatilia sana yanayotokea kule Kagera na naendelea kufuatilia kwa sababu jamaa zetu wa kule kwa kweli wanahitaji msaada wetu ingawa na wao pia wanapaswa kuchukua hatua zao na za jamaa zao wa karibu katika kujinasua na janga lililowafika.

Maoni yangu leo si ya kueleza tukio hilo wala kufafanua maafa yalivyowagusa ndugu, jamaa na marafiki zetu, bali kimsingi, nimeandika kufikisha ujumbe kwa Mhe Rais wa Awamu ya Tano, Dkt. John Pombe Magufuli. Nitaeleza kwa nini Dkt. Magufuli anapaswa kupewa hongera zake katika hili.

Mosi, tufahamu kuwa hili ni janga  la asili na ni jambo ambalo wanasayansi wanasema halitabiriki na hakuna mtu anaweza kujua lini tetemeko la ardhi litatokea. Lakini hata tukijua, bado ni ngumu kuzuia athari zake hasa kwa makazi na miundombinu.

Lakini tangu kutokea kwa jambo hili, labda tofauti na ilivyopata kutokea katika majanga mengine nchini kama vile mafuriko ya Kilosa na majanga mengine ya tetemeko au mafuriko, kwa mara ya kwanza, na ikiwa haina uzoefu bado wa muda mrefu katika uongozi, Serikali ya Magufuli imetuunganisha na imetutendea haki sana kwa kiwango chake.

Mara tu baada ya tukio, Waziri Mkuu alifika Kagera kuwajulia hali waathirika, kushiriki mazishi ya umma ya waliofariki na kutoa maagizo kwa watendaji wake juu ya hatua za haraka za kufanywa.

Mara tu baada ya Waziri Mkuu kutoka Kagera, Rais Magufuli ambaye hata baadhi ya watendaji wake waandamizi walishakuwa mjini Lusaka, Zambia alikokuwa aende kwa ajili ya sherehe za kuapishwa Rais Lungu, naye aliahirisha safari hiyo.

Rais aliahirisha safari na kubaki Dar es Salaam kuratibu kwa karibu maafa hayo na namna ya kuwasaidia waathirika. Na mara moja tuliona athari za uwepo wake nchini ambapo ilifanyika harambee Ikulu ambapo watanzania tukahamasishwa kuchangia.

Serikali ikachukua hatua muhimu za mawasiliano na hamasa kwa wadau ikiwemo kutangaza akaunti ya maafa na namba za simu za sisi kuchangia. Akaunti hizi, tofauti na miaka ya nyuma zimesambazwa sana katika mitandao ya kijamii na hata nimeona matangazo katika magazeti na katika televisheni. Mkuu wa Mkoa wa Kagera anatoa taarifa za mara kwa mara pia.

Serikali pia kupitia taasisi na wizara mbalimbali pia imeendesha matukio mengine ya kuchangia waathirika, imeratibu nchi nyingine za kigeni na Balozi kupeleka misaada Kagera na misaasa hiyo imeanza kuwafikia waathirika.

Nafahamu kuwa Serikali haikuwa na wajibu wa moja kwa moja katika hili kwa kuwa haikusababisha, lakini juhudi hizi ni za kupongezwa sana na za kukumbukwa sana. Mzee Magufuli Mungu akutangulie.

Nnitumie fursa hii pia kuwasihi watanzania wenzangu, katika kuwasaidia wenzetu, kama tulivyoanza, kusiwe tena na siasa wala watu kutafuta upungufu na kukosoa. Kila mmoja wetu “ajiongeze” wanasema vijana wa  mjini.

Hata kwa ndugu zangu waathirika nao pia tujue sisi na jamaa zetu tuna jukumu la kwanza katika hili na tujitume kujinasua katika janga hilo, Serikali inaweza kuleta kidogo cha kuchangia au kutufuta machozi, au kurekebisha miundombinu ya umma lakini tusibaki watu wa kusubiri tukidhani ndio tutafanyiwa kila kitu.

Hakuna Serikalini duniani inayoweza kufanya kila kitu hasa yanapotokea majanga makubwa hata ziwe na uwezo vipi. Niliwahi kufika Marekani kwenye eneo la janga la Septemba 11 pale Manhttan, New York na kukuta hata baada ya miaka 10 eneo lile halikuwa limeweza kurejea katika hali yake ya awali.

Kuna eneo kule Japan baada ya maafa ya mafuriko nimepata kuvikuta vikiwa hadi leo haviko katika sura yake ya awali. Naamini hata ndugu zangu wa Kagera wajue hili, yapo mambo yanaweza kufanyika yakawa bora zaidi kwa jitihada zao na za Serikali, lakini pia yapo yanayoweza kuchukua muda zaidi na au hata yasirejee katika hatua kama za awali.

Nihitimishe, hongera kwa JPM lakini pia Serikali na wadau wengine tuendeleze moyo huu huu na ushirikiano huu huu katika matukio mengine mengi zaidi yawe ya maafa au ya kawaida. Kama tulivyoungana katika suala la madawati na hili la maafa, naamini tukiendelea kuungana pamoja, Tanzania itasonga mbele.

Nawashukuru sana.

MAMBO 10 YALIYONIGUSA KATIKA MUSWADA WA HABARI.

Na. Joseph Sabinus, Nottingham University
JUZI niliandika makala kuonesha kuwa kelele zinazoendelea kuhusu Muswada wa Sheria ya Huduma za Habari ukizitazama kwa undani utakubaliana nami kuwa ni matokeo ya kada isiyojiamini.
 
Tasnia ya habari hapo nchini haijiamini na hili linaweza kuelezwa ama na miaka mingi ya kuhangaika kuwa na sheria yao huku zoezi hilo kila mara likikumbwa na sababu mbalimbali na kuahirishwa au kwa namna wanavyojenga hoja zao.
 
Hata hivyo ukiziacha kelele hizo na kuanza kuusoma muswada huu kwa kina na kwa kutafakari makosa mengi yanayofanywa na vyombo vya habari popote duniani utakubaliana nami kuwa muswada huu, kama walivyosema pia Tanganyika Law Society na Twaweza, una mambo mengi mazuri na ni bora zaidi kuliko ile ya awali.
 
Nilidhani wanahabari wangeshiriki vyema katika kuboresha yale maeneo yenye changamoto badala ya kuwaachia watu wa tasnia nyingine. Ni bahati mbaya wadau hawa wamechagua kuwa wanaharakati zaidi badala ya wanataaluma.  
  
Binafsi baada ya kuusoma muswada nimebaini masuala makubwa yafuatayo katika hili. Naomba tushirikiane.  
 
1.     Sheria kutosajili mitandao
Awali nilipomsoma Mbunge Zitto Kabwe nilistushwa kusikia kuwa sheria hii inalenga kubana hadi mitandao ya kijamii. Hata hivyo sheria haisomwi kama gazeti.

Wakati Zitto alikuwa akisoma tafsiri ya neno “media” na kuona limejumuisha mpaka mitandao ya kijamii, ukweli ni kwamba ukiusoma muswada ule eneo ambalo sheria itahusika nalo kwa maana ya uratibu ni sekta iitwayo “print media”

Kwa hiyo ni kujidanganya kusema sheria hii itasajili mitandao ya kijamii na vitu vinavyofanana na hivyo. Badala yake ukisoma kifungu cha 8(1) unauona ukweli huu. Mitandao imekuwa kama chombo kingine cha habari lakini nadhani kuanza kuisajili sasa ni mapema mno.

2.     Habari ni taaluma
Kwangu mimi, sijui kwa wanahabari wenyewe, muswada huu unaleta kwa mara ya kwanza mfumo madhubuti wa kuifanya sekta ya habari kuwa taaluma kamili na itakayoheshimika na kutambuliwa zaidi.

Ukiutazama mfumo unaopendekezwa wa Bodi ya Ithibati katika ibara ya 10 utaiona “spirit” hii. Taaluma kuwa taaluma moja ya sifa ni hii. Lazima wanataaluma hiyo wawe na Bodi inayowasajili kwa viwango vilivyowekwa. Hata hivyo sijapata sababu kwa nini sifa hazijaanishwa kwa sasa.

3.     Bodi kumilikiwa na wanahabari
Wakati nikiendelea kuusoma muswada huu pia nilipatwa na wasiwasi kuhusu kuundwa kwa Bodi hiyo ya Ithibati nikidhani ingejaa warasimu tunaowafahamu siku zote.

Hata hivyo kama kuna jambo lingine la kuusifu muswada huu ni pamoja na muundo wa Bodi yake. Bodi itakuwa na wajumbe 7 na kati ya hao wanne (4) watakuwa ni wanataaluma ya habari akiwemo mwenyekiti wa Bodi.

Haya ni mapinduzi makubwa katika uundaji wa Bodi za kitaaluma ambapo katika maeneo mengine ingezingatiwa tu uwakilishi labda wa jinsi, umri au taasisi. Katika hili tuwapongeze waliosanifu muundo wa Bodi hii.

4.     Bara Huru lenye meno
Hapa nianze kwa kusema muswada huu umechelewa sana na hakuna hoja wala haja ya kusubiri tena. Wananchi wanahitaji kuhudumiwa na sekta bora zaidi ya habari na kila mmoja wetu anajua umuhimu huu.

Ukisoma kifungu cha 23 na kuangalia majukumu yale ya Baraza Huru la Habari utakubaliana nami kuwa tunahitaji Baraza hili Huru kuliko wakati wowote. Hilo Baraza linalotajwa kuwepo ni NGO tu na Serikali yoyote duniani haiwezi kuendeshwa na NGO.

Baraza linaloundwa humu nimeona litakuwa na uhuru na haki ya kutunga kanuni za maadili za wanahabari na kuhakikisha wenyewe wanazielewa katika kuwasimamia kwenye kazi zao. Hii ni muhimu sana.

Ukienda Mahakamani inachukua miaka. Ukienda MCT ya sasa hata wakitoa uamuzi chombo cha habari kinakuwa na uhuru wa kuukataa au kuukubali uamuzi huo. Baraza hili kwa kuwa limeanzishwa kisheria na lina nguvu za kisheria litakuwa na uwezo wa kusimamia hata utekelezaji wa hukumu zake.

5.     Wanahabari kutunga kanuni zao
Katika hili niseme tu kwamba kama kuna jambo wanahabari wamekuwa wakilikosa kwa muda sasa ni kwanza kuwa na chombo kimoja kinachowaunganisha bila kuwabagua zaidi ya wao tu kuwa wanahabari.

Katika Baraza linaloanzishwa nimeona vifungu kuwa litakuwa na kazi nyingine muhimu na ya kipekee (exclussive rights) ya kuandaa kanuni za maadili (media code of ethics). Hii ni muhimu kwa sababu badala ya kutungiwa na watu wengine ni wanahabari wenyewe watakaozitunga kwa sababu pia wanafahamu vyema kazi yao.

6.     Kamati ya malalamiko
Kumekuwa na fikra miongoni mwa watu kuwa kuipata haki mahakamani ni gharama kubwa sana na inayochukua muda mrefu. Katikati ya keleleza za baadhi ya watu kuwa sheria hii haina jema, ni muhimu kuona umuhimu wa kifungu hiki.

Kwa kuanzishwa Kamati ya Malalamiko chini ya Baraza Huru la Habari, sasa wananchi watapata pa kulalamikia na tena penye meno. Lazima tukubali kuwa ama kwa ajenda fulani au makosa ya kibinadamu, vyombo vya habari nchini vinawakosea sana watu binafsi au taasisi.

Naamini ni vyema kuwapa wahusika mahala pa kulalamika kwa sababu kwenda Mahakamani ni suala ambalo kila mmoja, kwa sababu tulizokwishaeleza, asingependa kulichagua. Kamati hii basi ikiundwa itoe uamuzi kwa haraka na iwe madhubuti.

7.     Bima ya Afya
Mwezi Novemba mwaka jana nilirejea nchini kwa mapumziko ya mwisho wa mwaka. Katika pita pita zangu jijini Dar es Salaam nilikutana na matukio mawili ya wanahabari kuchangiwa na wenzao.

Nilipofuatilia suala hili nikaambiwa kuwa wanahabari hao hawakuwa na bima na walipopatwa na maradhi ya muda mrefu ikawalazimu kuishi na kupata tiba kupitia michango ya kujitolea ya wanataaluma wenzao.

Wapo pia waandishi ambao hadi sasa wako hai lakini wanaishi kwa kutegemea misaada ya ndugu na jamaa kwa ajili ya kupata huduma za afya. Nauona muswada huu unakuja kuwakomboa wanahabari. Ni muswada unaokuja kuhakikisha kuwa si tu wanataaluma hii wanafanya kazi zao kwa ufasaha lakini pia waweze kupata haki yao ya matibabu na kuwekewa hifadhi ya jamii.

Iliniuma na leo tunapoona katika kifungu cha 58 cha muswada huu kuna ulazima kwa wamiliki wa vyombo vya habari kuwakatia bima watu wao, inashangaza kuona wapo wanahabari ambao wanadai muswada huu haufai na kutaka urejeshwe nyuma.  

8.     Haki za watu
Ukisoma Tamko la Haki za Binadamu la 1948 utaona msingi wa haki kuwa umebebwa katika dhana ya haki ya mtu mmoja hukoma pale utekelezaji wa haki hiyo unapoingilia uhuru au haki ya mtu mwingine.

Nimeviona vifungu kadhaa vya muswada huu vikiwa na mlengo huu wa kuhakikisha wakati, kwa mfano, haki ya wanahabari kukusanya na kusambaza habari ikiwa ni muhimu, pia ziko haki za watu wengine zinazopaswa kulindwa na wanahabari.

Kifungu cha 32 katika hili kwa mfano kinaainisha au kukataza waandishi kuchapisha kashifa na kuwashushia watu wengine hadhi zao bila sababu (wawe hai au wamekufa). Hii ni muhimu sana.

9.     Usalama wa Nchi
Nikikumbuka jinsi vyombo vya habari vilivyochangia katika machafuko katika nchi mbalimbali duniani hasa Rwanda (1994) na Kenya (2007) nashawishika kuchekelea ninapousoma muswada huu.

Ukiacha vifungu vinavyoainisha uchochezi, nimeguswa zaidi na kifungu cha 55 cha Sheria kinapompa mamlaka Waziri akijiridhisha kuwa kuna suala linalokwenda kukiuka usalama wa nchi basi achukue hatua haraka.

Wanaharakati hupinga vifungu kama hivi kwa hoja za juu juu tu za kutokuwaamini viongozi wanaoweza kupewa madaraka hayo, lakini uhalisi kwamba mambo haya yameshatokea na kwamba zipo nchi zimeshawahi kuingia katika umwagaji wa damu kwa vyombo vya habari kuachwa huru watakavyo, mtu hawezi kubeza kuwekwa kwa vifungu kama hivi.

Lipo pia kosa la uchochezi ambalo wengi, bila kulitafakari, wanapiga kelele zilizokosa tafakuri. Unawezaje kuwaacha watu watumie vyombo vya habari kuchochea vurugu, kuhamaisha uasi na machafuko katika nchi? Kwangu mimi makosa kama haya ni muhimu kwa usalama wa nchi na ni juu ya kila mmoja kutekeleza sheria.

10.   Kufutwa sheria ya Magazeti
Mimi nikiwa hapo nyumbani kwa miaka mingi nimekisikia kilio cha wadau dhidi ya Sheria ya Magazeti, 1976. Sheria hii tumekua nayo, tumeishi nayo na tulianza kuzeeka nayo lakini kila mwanataaluma akijua haikuwa sheria nzuri.

Kwamba leo inafutwa ni faraja kwa tasnia na nilidhani wenzetu wengine badala ya kulaani jambo hili wangeungana nasi kulishangilia. Kwangu, kama kuna jambo jingine kubwa kwa wanatasnia kulishangilia ni kufutwa kwa sheria hii ambayo wengine walifikia hatua ya kuiita “ya kikatili.”

Wakati nikiamini wabunge watakuwa wamefanyiakazi changamoto nyingine na kuuboresha muswada katika maeneo machache kama vile kukamatwa mitambo kabla ya uamuzi wa mahakama na kuainishwa viwango vya taaluma, niwaase wanahabri nchi kuwa katika ulimwengu wa utatuzi wa migogoro; mazungumzo ni muhimu.

Ni bahati mbaya kwamba katika hili walichagua kutozungumza na Kamati ya Bunge na wakasusia na hatimaye muswada huu ukipita utawahusu hata kama wao hawakushiriki kuutunga.

*Mwandishi wa makala haya amejitambulisha kuwa ni mwanafunzi wa shahada ya uzamivu (PhD) kwenye Chuo Kikuu cha Nottingham, Uingereza.

BUNGE LAIGOMEA SERIKALI KUSAINI EPA.

Na Mwandishi Wetu–Dodoma

Mkutano wa Tano wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania umeizuia Serikali kusaini Mkataba wa Makubaliano ya Ushirikiano wa Kiuchumi Kati ya Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) na Jumuiya ya Ulaya (EU) – (EPA) kwa kuwa hauna manufaa kwa nchi ya Tanzania.
Uuamuzi huo umetolewa leo mjini Dodoma na wabunge wa Bunge hilo baada ya kuujadili mkataba huo kwa kina kwa kutoa maoni yao ambapo wengi wameunga mkono kutosainiwa kwa mkataba huo.

 
Baadhi ya wabunge waliopata nafasi ya kutoa maoni yao katika mjadala huo ni pamoja na mbunge wa Mtwara Vijijini, Mhe. Hawa Ghasia ambaye amemshauri Mhe. Rais Dkt .John Pombe Magufuli kutosaini mkataba huo kwa kuwa una hasara nyingi kwa taifa kuliko faida.
”Kwa kuzingatia mkataba umeruhusu uingizaji na utoaji wa bidhaa huru na ukizingatia hakuna nchi hata moja ya Ulaya ambayo Tanzania inapeleka bidhaa zake hivyo mkataba huu hauna maslahi kwa watanzania”, alisema Mhe. Ghasia.
Aliongeza kuwa Tanzania sio nchi ya kwanza kutosaini mkataba huo kwani kuna nchi kama Angola, Nigeria, na Gambia hazijasaini,ameongeza kuwa kama Tanzania itakubaliana na mkataba huo utaua viwanda pamoja na biashara za Tanzania.
Kwa upande wake Mbunge wa Nzega Mjini (CCM), Mhe.Hussein Bashe alisema kuwa tatizo lililopo katika mkataba huo ni kutoitambua nchi kama nchi na badala yake kuangalia nchi zote kwa pamoja hivyo amewashauri wabunge kuhoji kuanzia kwenye kiini cha tatizo.
“Kwa kuwa kifungu cha 143 cha mkataba huo kinaruhusu kupeleka marekebisho, naishauri Serikali yetu ipeleke marekebisho ya kupendekeza kila nchi iingie mkataba kivyake kulingana na maslahi ya nchi yake”, alisema Bashe.
Aidha, Mbunge wa Mwibara Mhe.Kangi Lugola (CCM) alimpongeza Mhe. Rais Magufuli kwa kusita kusaini mkataba huo kwani ni miongoni mwa mikataba mibovu kati ya mikataba iliyowahi kuletwa nchini kutoka katika nchi za Ulaya.
“Kama tukikubali kusaini mkataba huu nchi hii itakuwa dampo la bidhaa mbalimbali za ajabu kutoka nje na hivyo kupelekea kushindwa kutimiza dhamira ya nchi ya kuimarisha viwanda vyetu”, alisema Mhe. Lugola.
Naye, Mbunge wa Mchinga Mhe. Hamidu Bobali alisema kuwa mkataba huo haufai kwa maslahi mapana ya taifa hili kwani unataka kuondoa ushuru kwa bidhaa zinazoingia nchini wakati nchi ya Tanzania inaingiza bidhaa nyingi kutoka nje kuliko kupeleka bidhaa nje ya nchi.
“Kama tukikubali tukaondoa ushuru wa kuingiza bidhaa kutoka nje basi tutapoteza mapato mengi yanayotokana na kuwepo kwa bandari pia tunatakiwa tujiulize kama mkataba umeruhusu uingizaji na utoaji wa bidhaa huru je nchi yetu ina bidhaa zinazokidhi vigezo vya kuingia katika nchi za Ulaya?” , alihoji Mhe. Bobali.
Mhe. Bobali ametoa rai kwa Serikali kuileta Bungeni mikataba mikubwa kama ya gesi na madini kwa ajili ya kujadiliwa kwa kina ili kuepuka kusaini mikataba isiyo na tija kwa Taifa.
Baada ya majadiliano hayo hatimaye Bunge limepitisha Azimio la kuitaka Serikali kutosaini mkataba huo kwa sababu umeonekana kuwa na mapungufu yanayohitaji marekebisho ambayo yataleta maslahi kwa Taifa.

MAGUFULI GETS "STOP ORDER" FROM NATIONAL ASSEMBLY ON EPA.

By. Staff Reporter, Dar es Salaam
 
ATTEMPTS by the fifth phase government of Tanzania under President John Pombe Magufuli to reconsider whether or not to sign the Economic Partnership Agreement (EPA) have been thwarted by the country’s National Assembly.
 
During the last East African Community Heads of States Summit in Dar es Salaam, the partner states allowed more time for consultations. Specifically, Tanzania, needed more time to reconsider the various options on the economic partnership.
 
But the resolution made by the country’s National Assembly in session in Dodoma to stop the government from signing the EPA agreement in its current form, means President Magufuli’s options are minimized.

Constitutionally, a resolution of the National Assembly as an important pillar of the government is a binding advisory, says a law Professor based in Dar es Salaam.
 

Reports from Dodoma reveal that most Members of the Assembly contributed against any move to sign the agreement. Most of them citing the lack of protection of local industries if the current EPA document is signed, said the Agreement has to undertake comprehensive amendments.

 
In July, 2016 the Kenyan Daily Nation newspaper quoted some European MPs as backing efforts not to sign the deal to allow more time for consultations.