Friday, December 16, 2016

MWILI WA BRIGEDIA JENERALI MHAIKI WAAGWA RASMI LEO.

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (katikati) akifuatana na Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa Dkt.Hussein Ali Mwinyi  (kushoto) na Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Tanzania Jenerali Davis Mwamunyange (kulia)wakati Rais alipofika leo katika Hospitali ya Jeshi la Wananchi JWTZ Lugalo Dar es Salaam kwa ajili ya kuuaga mwili wa Marehemu Brigedia Jenerali Cyril Ivor Mhaiki aliyekua Kamanda wa Brigedi ya Nyuki Zanzibar,aliyefariki juzi hospitalini hapo baada ya kuugua kwa muda mfupi.

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akitia saini kitabu cha kumbukumbu ya Marehemu Brigedia Jenerali Cyril Ivor Mhaiki, aliyekua Kamanda wa Brigedi ya Nyuki Zanzibar,ambae alifariki juzi katika  hospitali  ya Jeshi la Wananchi JWTZ Lugalo JIjini Dar es Salaam,baada ya kuugua kwa muda mfupi na kuagwa leo

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (katikati) Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa Dkt.Hussein Ali Mwinyi  (kushoto) na Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Tanzania Jenerali Davis Mwamunyange (kulia) wakiwa katika Kambi ya Jeshi la Wananchi Lugalo Dar es Salaam leo   kuuaga mwili wa Marehemu Brigedia Jenerali Cyril Ivor Mhaiki aliyekua Kamanda wa Brigedi ya Nyuki Zanzibar,aliyefariki juzi katika hospitali ya Jeshi la Wananchi JWTZ Lugalo, baada ya kuugua kwa muda mfupi.

Baadhi ya Maafisa wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania JWTZ waliofika leo katika hafla ya kuuaga Mwili wa Marehemu Brigedia Jenerali Cyril Ivor Mhaiki aliyekua Kamanda wa Brigedi ya Nyuki Zanzibar,aliyefariki juzi katika hospitali ya Jeshi la Wananchi JWTZ Lugalo, baada ya kuugua kwa muda mfupi,ambapo utaagwa leo katika Hospitali Lugalo Dar es Salaam.

Wananchi mbali mbali na jamaa waliofika leo   kuuagawa  Mwili wa Marehemu Brigedia Jenerali Cyril Ivor Mhaiki aliyekua Kamanda wa Brigedi ya Nyuki Zanzibar,aliyefariki juzi katika hospitali ya Jeshi la Wananchi JWTZ Lugalo Dar es Salaam, baada ya kuugua kwa muda mfupi.

Jeneeza lenye Mwili wa Marehemu Brigedia Jenerali Cyril Ivor Mhaiki  aliyekua Kamanda wa Brigedi ya Nyuki Zanzibar,aliyefariki juzi katika hospitali  ya Jeshi la Wananchi JWTZ Lugalo   Dar es Salaam,ukibebwa  na askari kupelekwa sehemu maalum ambapo utaagwa rasmi leo kabla kupelekwa kijijini kwao kwa mazishi.

Mawaziri wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar na Viongozi pamoja na Wazee wa Chama leo walijumuika na Maaskari wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania katika kuuaga Mwili wa Marehemu Brigedia Jenerali Cyril Ivor Mhaiki aliyekua Kamanda wa Brigedi ya Nyuki Zanzibar,aliyefariki juzi katika hospitali ya Jeshi la Wananchi JWTZ Lugalo Dar es Salaam, baada ya kuugua kwa muda mfupi.

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein alipokuwa akitoa heshima ya mwisho leo kwa mwili wa Marehemu Brigedia Jenerali Cyril Ivor Mhaiki aliyekua Kamanda wa Brigedi ya Nyuki Zanzibar,aliyefariki juzi katika hospitali ya Jeshi la Wananchi JWTZ Lugalo Dar es Salaam, baada ya kuugua kwa muda mfupi.


No comments:

Post a Comment