Na. Genofeva Matemu.
Watayarishaji wa kazi za ubunifu ikiwemo filamu Tanzania wamehaswa kuwa wabunifu na kuacha kunakili kazi ambazo zilishafanywa na watu wengine kwani kwa kufanya hivyo hupelekea kudidimiza sekta ya Filamu na kuidhalilisha tasnia ya uigizaji nchini.
Watayarishaji wa kazi za ubunifu ikiwemo filamu Tanzania wamehaswa kuwa wabunifu na kuacha kunakili kazi ambazo zilishafanywa na watu wengine kwani kwa kufanya hivyo hupelekea kudidimiza sekta ya Filamu na kuidhalilisha tasnia ya uigizaji nchini.
Kauli
hiyo imetolewa na Katibu Tawala Mkoa wa Mara Bw. Ado Mapunda alipokua akifunga
warsha ya mafunzo ya kuwajengea uwezo wadau wa sekta ya filamu na michezo ya
kuigiza iliyofanyika kwa siku tatu na kufungwa leo Mkoani Mara.
“Tumieni
fursa hii ya kipekee kuchota maarifa ya kutosha yatakayowaongezea ujuzi katika
kazi zenu za filamu. Naamini baada ya warsha hii mtalenga kutoa kazi bora
zitakazokidhi mahitaji ya wadau wenu na pia zitakazoweza kushindana kwenye soko
la ndani na kimataifa” amesema Bw. Mapunda
Kwa upande wake Naibu
Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Bibi. Nuru Millao ameiomba
Ofisi ya Mkoa wa Mara na Wilaya zake kushirikiana na kuhimiza Sekta ya
Utamaduni kutengewa fedha kwa ajili ya maendeleo ya Filamu huku wakijumuishwa
katika fursa mbalimbali ikiwepo mikopo kupitia mfuko wa vijana na wanawake
ambapo itasaidia vijana na wanawake wengi
ambao wanajishughulisha na Tasnia ya filamu Kwa kuwa filamu inaweza kuchangia
ustawi wa uchumi kwa mtu mmoja mmoja na pia kuchangia pato la nchi kwa kiwango
kikubwa.
Naye katibu Mtendaji Bodi ya Filamu Bibi. Joyce
Fisoo amewaomba watayarishaji wa kazi za filamu kuwasilisha miswada yao kabla
ya kuandaa filamu zao ili bodi ya filamu ipate fursa ya kupitia miswada hiyo na
kuiboresha kabla ya filamu kuandaliwa jambo ambalo litasaidia kuondokana na
filamu zitakazokua zinazuiliwa kutokana na makosa madogo madogo yanayojitokeza
katika filamu zao.
Aidha
watayarishaji wa Mkoa wa Mara wametakiwa kutumia maarifa ya warsha hiyo
kutengeneza filamu zinazohamasisha uwajibikaji, umuhimu wa elimu kwa mtoto wa
kike, athari za ukeketaji, athari za uvuvi haramu kama baadhi ya maeneo ambayo
jamii ya Mkoa wa Mara inahitaji kuelimisha na kuondokana na dhana potofu.
Mafunzo
hayo yameshirikisha zaidi ya wadau wa sekta ya filamu na michezo ya kuigiza 200
kutoka Mkoa wa Mara, Halmashauri ya Manispaa ya Mosoma, Musoma Vijijini, Bunda
Mji, Tarime Mji, Halmashauri ya Wilaya ya Tarime, Lorya, Butihama na wadau
kutoka Mkoa jirani wa Simiyu.
No comments:
Post a Comment