Monday, January 2, 2017

ANTI-CYBER CRIME ACT PETITION QUASHED

THE petition seeking to declare unconstitutional the Cyber Crime Act enacted by Parliament in 2015 to provide protection of the national economy, financial services against cybercrimes and provide mechanism and framework of combating such crimes in Tanzania, has crumbled.
 This follows the decision of the High Court to reject the petition lodged by Mr Jebra Kambole to challenge several provisions of the Act, alleging that they violated his rights to seek, receive and disseminate information guaranteed under the Constitution of United Republic of Tanzania.
In their judgment delivered recently, a panel comprising Judges John Ruhangisa, Winfrida Korosso and Lugano Mwandambo ruled that the grounds advanced by Mr Kambole, who also serves as an advocate of the High Court, attacking 18 provisions under the Cybercrimes Act, lacked merits.
The grounds upon which the petitioner had relied ranged from subjective and arbitrary interpretation and application of the Cybercrimes Act by law enforcement organs, infringements of rights to privacy, restriction of the freedom of communication and the right to be heard.
He had complained that lack of interpretation of words used in some of provisions under the Act, notably unlawfully, intentional, unauthorised person, or data, information, or access could lead to arbitrary arrest and unjustified actions by the law enforcement organs on various offences.
The judges, however, stated: “We are of the view that looking at the said Act objectively one will not fail to find sections which define and describe offences. The sections provide for ingredients of offence and the sentence for each of offences.
The provisions cannot be widely drafted to net everyone.” They ruled that sections 4, 5,6,7,8,9,14,19, 21 and 22 of the Act complained of by the petitioner fall within the parameters of Article 17 (2) of the Constitution of United Republic of Tanzania and therefore they could not be construed to be repugnant to or inconsistent with such Article of the parent law.
The judges pointed out that an individual who is aggrieved by any decision by a public officer related to the implementation of the said provisions in the Act has recourse through judicial review where a public officer has acted unlawfully or beyond his powers in exercising his duties.
“Having so found we see no merits in the petitioner’s contention that the (said) provisions of the Act are inconsistent with spirit of Articles 17 (2), 29 (5) and 30 (2) of the Constitution.
We thus decline the invitation to hold as we hereby do that the provisions are unconstitutional as prayed,” they declared.
The petitioner had also challenged the provisions of sections 38 and 50 of the Act that they violated Articles 13 of the Constitution over the right to be heard. He had contended that section 38 allows any application by an authority for a hearing in court to be made exparte (in absence of the adverse party).
In the judgment, however, the judges noted that matters envisaged under section 38 of the Act relate to search and seizure, disclosure of data, expedited preservation, disclosure and collection of traffic data and content data. According to them, such matters cover at investigation stage.
“Under such circumstances, we are, with due respect, unable to see any merit in the petitioners’ argument because we do not think that investigation is the final stage in determining the rights of the said individual or service provider where the said data is retrieved from,” they said.
On the contrary, the judges said, it appears to accord with reality that the said person or service provider would have time to explain and defend on the content of the said data during a trial hearing if the case is brought for trial.
“In consequence, we hold that the provision of section 38 of the Cybercrimes Act Fall within the ambit of Article 30 (2)(b) of the Constitution since it is squarely for the purpose of protecting interests of public safety and public order by reason and therefore not violate of the Constitution,” they held.
Regarding section 50 of the Act, which empowers the Director of Public Prosecutions (DPP) to compound some offences committed without due considering to the need of the suspect, the judges agreed with the petitioner that it curtails the right to be heard under Article 13 (6) (a) of the Constitution.
They noted that the actions by the DPP are given finality and not amenable to appeal if a suspect voluntarily confessed commission of the offence and such actions are given the status of the High Court order on one part, but on the other part are unique in sense that the aggrieved person could not appeal. “We find this to be an anomaly.
Exercising powers vested in this court by Article 30 (5) of the Constitution and section 13 (2) of the Basic Rights Duties and Enforcement Act, we direct the government through the Attorney General within the period of 12 months to correct the anomaly.

Sunday, January 1, 2017

LOWASA ANZA NA KALI YA MWAKA 2017


Wakati Rais Magufuli akianza kwa kuendelea kujenga nidhamu aliyekuwa mgombea wa Chadema ameonekana kuzidi kuchoka kisiasa.

Katika salama zake za mwaka mpya kupitia Azam amesikika akishauri eti vijana waruhusiwe kufanya mapenzi.

Watazamaji kadhaa wamekuwa wajiuliza mzee huyu anamaana gani.

Kwanza ana maana gani? Kwamba watu wamezuiwa?Na nani?Lakini Je anamwambia nani awaruhusu?

Je alikuwa anaelewa anachokisema au network ilikata??

BOFYA HAPO CHINI KUMSIKILIZA ALICHOKIONGEA



Sunday, December 18, 2016

BREAKING NEWS!!

Diwani wa Chadema Kata ya Boma Jimbo la Mafinga Mjini ndugu Kisoma amesimamishwa  Udiwani na Tume ya Uchaguzi ya Taifa baada ya kuthibitika hajui kusoma na kuandika.

Friday, December 16, 2016

SERIKALI IMEJIPANGA KUHAKIKISHA SEKTA YA KILIMO INATOA MCHANGO KATIKA KUFIKIA NCHI YENYE UCHUMI WA VIWANDA

Na.Immaculate Makilika.

SERIKALI kupitia Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi imesema kuwa imeandaa mikakati mbalimbali  ili kuhakikisha Sekta ya Kilimo  inatoa mchango zaidi katika kufikia nchi ya uchumi wa kati.

Akizungumza Jijini Dar es Salaam jana katika kipindi cha TUNATEKELEZA kinachoandaliwa na kituo cha televisheni cha TBC, aliyekuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo ambaye sasa ni Katibu Mkuu  Wizara ya Ulinzi Dkt. Florence Turuka alisema kuwa Serikali imeandaa mikakati hiyo ili kuhakikisha kunakuwepo na uzalishaji wa mazao ya kilimo ili viwanda viweze kupata malighafi, chakula cha kutosha pamoja na ajira kwa wananchi.

“Serikali imeamua kuanzisha viwanda vidogo vya kuchakata mazao kwa ajili ya soko, kushirikisha sekta binafsi katika kuongeza thamani ya mazao, ili kuvutia wakekezaji katika sekta ya kilimo  nchini” alisema Dkt. Turuka.

Kwa mujibu wa Dkt. Turuka alisema ili kuhakikisha huduma za ugani zinakua za kisasa   Serikali inadhamiria kutumia simu za mkononi zitakazorahisisha utoaji wa  taarifa kwa wataalamu wa kilimo, ikiwa ni pamoja na kusaidia wakulima kupata huduma za kitaalamu kwa wakati.

Aidha Dkt. Turuka alisema mikakati mingine inayotekelezwa na  Serikali ni pamoja na kuongeza idadi ya  matrekta hadi kufikia 6,000 badala ya 400 yaliyokuwepo awali.
Aliongeza kuwa Serikali imekusudia pia kujenga maghala karibu na maeneo yanayozalisha mazao ya matunda na mbogamboga ili kuweza kuyahifadhi kwa muda kabla mazao hayo hayajapekelekwa sokoni ili kupunguza uharibifu.

Naye Katibu Mkuu wa sasa wa Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi, Mhandisi Mathew Mtigumwe alisema Serikali itaboresha mfumo wa takwimu wa wataalamu wa kilimo pamoja na kuwajengea uwezo ili kusaidia utekelezaji wa maendeleo ya kilimo katika maeneo mbalimbali nchini.

Aidha, Serikali inawakaribisha wawekezaji wa kilimo cha miwa ambapo imeandaa zaidi ya hekta 6000 kwa ajili ya kilimo hicho nchini.

WATAYARISHAJI FILAMU WATAKIWA KUWA WABUNIFU.

Na. Genofeva Matemu.

Watayarishaji wa kazi za ubunifu ikiwemo filamu Tanzania wamehaswa kuwa wabunifu na kuacha kunakili kazi ambazo zilishafanywa na watu wengine kwani kwa kufanya hivyo hupelekea kudidimiza sekta ya Filamu na kuidhalilisha tasnia ya uigizaji nchini.

Kauli hiyo imetolewa na Katibu Tawala Mkoa wa Mara Bw. Ado Mapunda alipokua akifunga warsha ya mafunzo ya kuwajengea uwezo wadau wa sekta ya filamu na michezo ya kuigiza iliyofanyika kwa siku tatu na kufungwa leo Mkoani Mara.

“Tumieni fursa hii ya kipekee kuchota maarifa ya kutosha yatakayowaongezea ujuzi katika kazi zenu za filamu. Naamini baada ya warsha hii mtalenga kutoa kazi bora zitakazokidhi mahitaji ya wadau wenu na pia zitakazoweza kushindana kwenye soko la ndani na kimataifa” amesema Bw. Mapunda

Kwa upande wake Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Bibi. Nuru Millao ameiomba Ofisi ya Mkoa wa Mara na Wilaya zake kushirikiana na kuhimiza Sekta ya Utamaduni kutengewa fedha kwa ajili ya maendeleo ya Filamu huku wakijumuishwa katika fursa mbalimbali ikiwepo mikopo kupitia mfuko wa vijana na wanawake ambapo itasaidia vijana na wanawake  wengi ambao wanajishughulisha na Tasnia ya filamu Kwa kuwa filamu inaweza kuchangia ustawi wa uchumi kwa mtu mmoja mmoja na pia kuchangia pato la nchi kwa kiwango kikubwa.

Naye katibu Mtendaji Bodi ya Filamu Bibi. Joyce Fisoo amewaomba watayarishaji wa kazi za filamu kuwasilisha miswada yao kabla ya kuandaa filamu zao ili bodi ya filamu ipate fursa ya kupitia miswada hiyo na kuiboresha kabla ya filamu kuandaliwa jambo ambalo litasaidia kuondokana na filamu zitakazokua zinazuiliwa kutokana na makosa madogo madogo yanayojitokeza katika filamu zao.

Aidha watayarishaji wa Mkoa wa Mara wametakiwa kutumia maarifa ya warsha hiyo kutengeneza filamu zinazohamasisha uwajibikaji, umuhimu wa elimu kwa mtoto wa kike, athari za ukeketaji, athari za uvuvi haramu kama baadhi ya maeneo ambayo jamii ya Mkoa wa Mara inahitaji kuelimisha na kuondokana na dhana potofu.

Mafunzo hayo yameshirikisha zaidi ya wadau wa sekta ya filamu na michezo ya kuigiza 200 kutoka Mkoa wa Mara, Halmashauri ya Manispaa ya Mosoma, Musoma Vijijini, Bunda Mji, Tarime Mji, Halmashauri ya Wilaya ya Tarime, Lorya, Butihama na wadau kutoka Mkoa jirani wa Simiyu.

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI.

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amemuagiza Mkuu wa Wilaya ya Ngorongoro, Bw. Rashid Taka na Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo Bw. Raphael Siumbo kufanya uchunguzi na kuwachukulia hatua watendaji wote watakaobainika kuhusika katika uuzwaji wa kiwanja cha shule ya msingi Waso.
Ametoa agizo hilo jana jioni (Alhamisi, Desemba 15, 2016) wakati akihutubia wananchi katika mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye kata ya Waso Wilaya ya Ngorongoro akiwa katika ziara ya kikazi mkoani Arusha.
Waziri Mkuu alisema Serikali haiwezi kuvumilia kuona watendaji wachache wasiokuwa waadilifu  wanamega kiwanja cha shule na kukiuza kwa maslahi yao, hivyo aliwataka viongozi hao kufuatilia na kumpa taarifa ya hatua za kisheria walizochukua kwa wahusika.
“Mkuu wa wilaya na Mkurugenzi hapa kuna malalamiko ya viwanja fuatilieni viwanja hivyo vinavyolalamikiwa na wananchi ni viwanja gani je hiyo ya kwamba mmeuza viwanja vya shule ameuziwa nani,” alisema.
Aidha, Waziri Mkuu amemtaka Bw. Taka ahakikishe Mkuu wa Idara ya Ardhi, Maliasili na Mzingira, Bw. Switbeth Byorushengo anatekeleza majukumu yake ipasavyo. Ametoa agizo hilo baada ya wananchi kudai Ofisa huyo ameshindwa kufanya kazi na kumuomba Waziri Mkuu aondoke naye.
Alisema Bw. Byorushengo anatakiwa kuhakikisha halmashauri hiyo inapima viwanja vya kutosha na kutoa hati kwa wananchi ili waweze kupata maeneo ya kujenga makazi na shughuli zingine za kijamii.
Katika hatua nyingine, Waziri Mkuu alimuagiza Mkurugenzi wa halmashauri hiyo Bw. Byorushengo kuhakikisha halmashauri hiyo inaanza ujenzi wa hospitali ya wilaya na ifikapo Aprili, 2017 awe amepewa taarifa za ulipofikia ujenzi huo.
Kwa upande wake Mkurugenzi huyo alisema tayari wapo katika mchakato wa ujenzi wa hospitali ya wilaya ambapo wametenga sh. milioni 800 za kuanzia.
Akizungumzia kuhusu mgogoro wa ardhi kati ya vijiji vya Tarafa ya Loliondo na Hifadhi ya Taifa ya Serengeti, Waziri Mkuu alitoa muda wa siku 30 kwa uongozi wa Shirika la Hifadhi za Taifa Nchini (TANAPA) wawe wamekamilisha uhakiki wa mpaka huo.
Naye Naibu Waziri wa Kilimo, Mifugo na Uvuvi ambaye ni Mbunge wa Ngorongoro Mheshimiwa William Ole Nasha alimuomba Waziri Mkuu kuwasaidia kutatua mgogoro huo wa ardhi kwa kuwa ni wa muda mrefu na unakwamisha shughuli za maendeleo.
Awali, Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Bw. Mrisho Gambo alisema Wilaya ya Ngorongoro inachangamoto nyingi ikiwemo ya ardhi na sasa kuna mgogoro kati ya Kampuni ya Thomson Safari na wananchi ambao wanadai kuwa ardhi hiyo ilichukuliwa kinyemela na mwekezaji huyo bila ya wao kushirikishwa.
Alisema baada ya ziara ya Waziri Mkuu kumalizika mkoani hapa atarudi wilayani Ngorongoro kwa ajili ya kutatua kero mbalimbali ikiwemo ya ardhi na matumizi mabaya ya fedha zinazotolewa na wawekezaji ambazo matumizi yake hayajulikani.
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,
IJUMAA, DESEMBA 16, 2016.